BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS

.......

.

Friday, May 21, 2010

KIPINDI CHA PLANET BONGO EATV CHAPOTOSHA UMMA(Pt II)

                Kwanza Abdalah hakujiandaa kutengeneza kipindi rasmi cha kuja kuishindanisha Mwanza na Arusha,kitu alichokifanya ni kutengeneza kipindi cha “bora liende” ili tu mwisho wa siku ionekana hakwenda Mwanza burebure,ni dhahiri alirekodi kipindi kabla ama baada ya show ya J-Martins,kwahiyo kulikuwa na haraka ya ama kuwahi mambo mengine ya msingi zaidi yaliyomfanya aende Mwanza au kuwahi kufanya haraka ya kujiandaa na safari ya Arusha kuendelea na tour ya J-Martins ambayo kiratiba ilikuwa ipigwe siku moja baada ya show ya Mwanza,na ndio maana aliweza kuzungumza na wasanii kutoka studio moja tu ambayo ni mpya na wasanii wote ma-underground na ambao hawana hata experience ya kuzungumza na MEDIA,Dullah alizungumza na producer SAMTIMBER na baadhi ya wasanii wanaofanyakazi katika studio za A2P Records,tukianzia na hapo, A2P Records sio studio ya mfano kwa MUZIKI wa Mwanza,ni studio ndogo bado,tena sana tu,kufanyakazi na baadhi ya wasanii kutoka hapa Dar haina maana tayari imekwishakuwa studio ya mfano,wasanii toka Dar hawajaanza leo kusafiri mpaka Mwanza kurekodi nyimbo,wameanza tangu enzi ENRICO yuko Mwanza akimiliki MWANZA RECORDS mwaka 2001.Kama Dullah alikuwa na nia ya kutengeneza kipindi Mwanza cha ushindani wa kweli angekwenda katika studio zenye muda kidogo Mwanza na kutengeneza kipindi hicho,mfano angekwenda basi MO RECORDS akaonana na producer Q ambaye sasa yuko huko baada ya kuondoka BONGO RECORDS,au angekwenda basi TETEMESHA RECORDS akapata nafasi ya kuiona studio ambayo imekwisha tengeneza HITS kibao ambazo zinachezwa kwenye redio stations kibao kila kukicha bila hata ya wapenzi wa muziki kujua kuwa kumbe nyimbo hizo zimetoka MWANZA,studio ambayo imewatoa wasanii kibao akiwemo HUSSEIN MACHOZI ambaye hakuna asiyemjua leo. Kuliko kufanya alichokifanya.
              Mbali na hivyo bado huwezi kupata ripoti ya ukweli KIMUZIKI kwa kuongea na producer mmoja tena mgeni na ma-undergroung wawili watatu,historia ya muziki wa eneo fulani huwezi kuipata hivihivi tu,ni lazima uvuje jasho kwa kuwatafuta WAZAWA halisi wa eneo husika,zungumza na watu wa MEDIA wenzio wa muda mrefu eneo hilo,zungumza na wasanii wa zamani wa eneo husika,zungumza na mapromota pamoja na malegendari mbalimbali katika kiwanda cha burudani katika eneo husika utapata ripoti sahihi,kitu ambacho huyu mshkaji wetu hakufanya hata kwa asilimia moja,ndo maana napata wasiwasi kwamba inawezekana PLANET BONGO sasa inaanza kumshinda Dullah.Vitu vyote hivyo vinahitaji maandalizi makubwa na ya muda mrefu,sio kuripuaripua,Dullah angefanya hivyo au la,angemaliza mtiririko wake kawaida bila kufanya mlinganisho KIMUZIKI kati ya Mwanza na Arusha.Kwa waliopata nafasi ya kuzungumzia tathmini kimuziki kati ya Mwanza na Arusha katika sehemu ya tatu ya exclusive hiyo, walimtolea mfano mwanamuziki H-BABA,ni vitu vya kuchekesha sana kwakweli,H-BABA ni mwanamuziki mzuri ila sio ishara ya muziki wa Mwanza japo ametokea Mwanza,H-BABA ni “kitukuu” cha muziki huu Mwanza.
                Mi nakumbuka back in a days,mwanzoni mwa miaka ya 1990 watu kama Hayati HAMAD aka TERMINATOR X(RIP),watu kama kina PAUL JAMES(PEE JAY) ambaye sasa ni mtangazaji wa Clouds na mwenzake YAQUB waliokuwa wanaunda kundi la GGV,Dj YUSUPH(yuko UK now),KASSIM MTINGWA(nduguye RUKIA MTINGWA wa VODACOM) na K-SOLO waliokuwa wanaunda kundi la WEPWAA(Wepesi Wa Akili) na makundi mengine kama III-DA FAD,II NATURE BOYS(lililomkuza FID Q) na baadae THA ROTTEN BROTHERS,BH MOBB(Toka Bugando Hill Side), G.W.A(Gangstars With Atitude),SWAHILI GENERATIONS(Toka Mlango Mmoja),CHICAGO WHITE SOX,KING KIFF NIGGA(mwandishi wa magazeti ya Sani,blogger pia),JONTWA JOKERI toka Pasiansi ambako ndo chimbuko la muziki wa Dancehall na Raggae Maffin(Ni mchungaji leo na anamiliki kanisa lake),RWEYMAN na SHIJA(RAGGEA NATION) na washkaji wengine kadha toka mikoa ya jirani kama BOB HAISA &SWEET K na jamaa flani walikuwa wanajiita PMD(PLUS MINUS DIVIDE) toka Shinyanga na wengine wengi ambao siwezi kuwataja wote hapa,hao ni baadhi ya malegendari wanaothibitisha kuwa muziki Mwanza umeanza kitambo na si juzijuzi kama inavyoonekana,wakati huo matamasha ya muziki huu yalikuwa yanafanyika GADHI HALL pale kwenye makutano ya barabara za Nyerere,Kenyatta na Makongoro,LIBERTY CINEMA mtaa wa Liberty na ukumbi wa sinema wa zamani ambao baadae ulikuja kuwa ukumbi wa disko TIVOL barabara ya Posta,baadhi ya malegendari wengine ambao hawakuwa wasanii lakini wadau wakubwa ni kama DAUDI NYALA(DAVID LATTAH) huyu ni mdogo wake na Mh.Antony Diallo,DJ ENGENEER(alikuwa MC wa matamasha karibu yote wakati huo),MARCO TIBASIMA,OSCAR MAKOYE(DJ OSCAR MARK),DJ MILIONARE(Jacob Usungu),DJ EDDY GRAND(Delux Disco),RENA CALIST(Promota),MC STOPA(Muhsein Mambo)na wengine kibao tu ambao wapo na wanaweza kupatikana kuthibitisha hilo.

0 comments: