BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS

.......

.

Friday, May 21, 2010

MNM'S ALBUM OF THE WEEK..."AMAZIN' BY TRINA...

Baada ya wiki iliyopita kumtembelea KING wa wote katika R&B huko mbele mtu mzima R-Kelly,na tukaichambua na kuitazama kwa pamoja albam yake ya sasa "UNTITLED", leo tunaweka usawa wa kijinsia kwa kumcheki mdada anaitwa KATRINA LAVERNE TAYLOR aka TRINA na mzigo wake unaotisha unaitwa "AMAZIN".Mwanadada huyu alizaliwa Dec 3 mwaka 1978 na sasa amekuwa nominated katika tunzo za BET katika category ya "The Best Female Hiphop Artist" 2010.Kihistoria Trina anatoka MIAMI Florida United States na amekulia katika maisha ya tabu sana,kimuziki alianza kusikika katika collabo na Tricky Daddy ngoma iliitwa "Nann Nigga" mwaka 1998,baadae akasaini Slip-N-Slide Records akaachia mzigo wake wa kwanza mwaka 2000 kwa jina "Da Baddest B***ch",baadae akaanza kuachia albams mwaka hadi mwaka kama "Diamond Princess"(2002),"No Patients"(2004),"Glamorest life"(2005),"Here We go Again"(2006) and "Still the Baddest"(2008).

TRINA

Amazin iliachiwa rasmi kitaa tar 4 mwezi huu wa tano,kwahiyo bado ni mpya kabisa na ndani una mikonoz kumi na tano minene mwanzo mwisho,kama "Thaz Ma Attitude", "Million Dolla Gal" feat; Keri Hilson&Diddy, "On Da Hush" feat; Shonie, "Dang a Lang" feat; Lady Saw&Nicki Minaj, "I want it all" feat; Monica Arnod, "White Gal" feat; Flo Rida&Git Fresh, "My Bitches", "By Myself", "Always" feat Monica, "Currency" feat Lil Wayne&Rick Ross, "Make way" feat; Lyfe Jennings, "Let Dem Hos fight" feat; Kalenna, "Showing Out" na "Carpricon".
DA BADDEST B***CH

Mzigo una urefu wa dk 56 na sekunde 25 na ni kutoka EMI,Slip-N-Slide na DP Entertainment,umepikwa na producers wakali wafuatao,Jim Jonsin,CP Hollywood,Travis Spicey,Mario Winanz,Oddz and Endz,Maxwell Smart,Cozmo na Schife&Ohzee.Nyimbo zilizotangulia ni "Thats my attitude" ulioachiwa Oct 17 mwaka jana,"Million Dolla Gal" ulioachiwa Jan 7 mwaka huu,"Always" ulioachiwa muda mfupi kabla mzigo haujadondoka kitaa na BONGE moja la ngoma lililonifanya nikuletee mzigo huu wiki hii "Currency" aliofanya na Lil Wayne na Rick Ross ambao ndo umeachiwa sasa hivi.Albam hii "AMAZIN" ya Trina iko nafasi ya 49 wiki hii katika Billboards Top 200 albums,niko chini ya miguu yako mdau na fans wa MNM,tafuta albami hii halafu tulia usikilize kwa makini,NI BONGE MOJA LA ALBAM.Thanx!

 
AMAZIN(COVER ALBAM)

0 comments: