BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS

.......

.

Friday, August 6, 2010

HAV A GUD WEEKEND FANS...LETS MEET ON MONDAY..

MNM'S ALBUM OF THE WEEK.."ELEMENT OF FREEDOM" By ALICIA KEYS"

ELEMENT OF FREEDOM(COVER)

Huu ni mzigo wa nne wa Alicia Keys Dean ambao uliachiwa rasmi Dec 11 2009 chini ya MBK na J Records..mzigo ulirekodiwa kuanzia May mpaka Sept 2009 ndani ya The Oven Studios pale Long Island, New York US..producers waliohusika ni pamoja na Alicia Keys mwenyewe, Jeff Bhasker, Swizz Beatz, Noah "40" Shebib na Kerry "Krucial" Brothers.Mdau mzigo huu ni noma..ni mkali balaa coz umekwenda mpaka nafasi ya pili kwenye US Billboard 200 Chart na kuuzwa zaidi ya nakala 417,000 wiki yake ya kwanza tu kitaa..

SWIZZ & ALICIA(LOV GON' GUD)

Kihistoria hii ndo albam yake ya kwanza kuuza kiasi hiki US na UK ..baada ya mwezi wa kwanza tu ukatukiwa platinum na RIAA japokuwa style ya Alicia ya kuimbia key ya chini(low key style) pamoja na uandishi wake ni vitu ambavyo vimekuwa vikisababisha mauzo yasiyoridhisha ya albams zake zilizopita..hii imekuwa tofauti kabisa..na mpaka June 8 2010 mzigo ulikuwa tayari umeshagongwa nakala 1,305,000 kwa Marekani tu.Mwenyewe alisema "nimetengeneza albam hii baada ya kupitia mengi magumu...ni kama kuondokana na mgandamizo wa moyo,najisikia huru sasa"..Singles zilizotangulia ni "Doesn't Mean Anything" ambao uliachiwa Sept 22 2009, "Try Sleeping With a Broken Heart" Nov 17 2009, "Empire State of Mind" pt II Feb 22 2010, "Un-Thinkable(Am Ready)" May 22 2010 na baadae ni "Put it in a Love Song" ambao utaachiwa mwezi ujao...

SWIZZ & MASHONDA(LOV GON' BAD)

Sasa check mikono iliyomo humo ndani..."The Element Of Freedom (Intro)", "Love Is Blind", "Doesn’t Mean Anything", "Try Sleeping With A Broken Heart", "Wait Til They See My Smile", "That’s How Strong My Love Is", "Unthinkable (I’m Ready)", "Love Is My Disease", "Like The Sea", "Put It In A Love Song" Feat. Beyonce, "This Bed", "Distance And Time", "How It Feels To Fly" na "Empire State Of Mind (Part II)"...Kama bado unasuasua kuutafuta na kuusikiliza mzigo huu...pole sana ndugu yangu.


ZINANIKUMBUSHA MBALI..."THE DIARY" By SCARFACE

THE DIARY(COVER)

Anaitwa Brad Jordan kwa jina halisi..ambaye wakati analitumikia kundi la Gheto Boys(sio lile la Afande Sele wa Moro) alikuwa anatumia Akshen..alizaliwa Nov 9 1969 Houston US..Huu ni mzigo wake wa tatu baada ya kuamua kufanya solo projects(hakujitoa kabisa kundini)..wa kwanza ulikuwa "Mr Scarface is Back" wa 1991...halafu "The World is Yours(face II face)" wa 1993..."The Diary" ambao aliuachia Oct 18 1994 ni moja kati ya mizigo ambayo inanikumbusha mbali ile mbaya nikiusikiliza..na huwa nikitaka kupumzisha akili yangu baada ya "stress" za hapa na pale za kimaisha nausikiliza mzigo huu,haunichosi aisii..


MY HOMMIES(COVER)

Una mikono 13 ukijumlisha na intro na outro ambayo ni "The White Sheet", "No Tears", "Jesse James", "G's", "I see a Man Die", "One", "Goin' Down", "One Time", "Hand of a Dead Body", "Mind Playin' Tricks" na "The Diary"..Producers waliotia mautundu yao huko ndani ni Scarface mwenyewe, Mike Dean, Ice Cube, Unkle Eddy na N.O.Joe..Def Jam ndo lebel husika japo baadae mchizi akaamua kuanzisha lebel yake Rap-A-Lot Records,baada ya hapo mchizi akawa anadondosha tu mizigo mikali kitaa..kama


THE WORLD IS YOURS(COVER)

"Untouchable"(1997).."My Hommies"(1998).."The Last of a Dying Breed"(2000)..."The Fix"(2002)..."Balls & My Word"(2003)..."My Hommies Pt II"(2006) ambayo haikufanya vizuri kama alivyotegemea kitu ambacho kilimfanya aungane na marapa flani wadogo Young Malice na Willie Hen na kuachia "One Hunid" mwaka huohuo 2006 na mzigo wake wa mwisho ni "M.A.D.E wa 2007.Ama kweli cha kale dhahabu(The Diary). 

Thursday, August 5, 2010

REGGAE BASH IRINGA TOWN...


Heshima zenu ndugu.



Nawakaribisheni tena kwenye mchakato mzima wa kukata kasi ya baridi hapa Iringa kwa kusakata mirindimo ya Reggae mwanzo mwisho kila jumapili. Pamoja sana.