LOVELY GAMBLE(MOVIE COVER)
Movie imetengenezwa na URBUN PULSE na imeshutiwa Uingereza,ndani kuna "galacha" wa filamu za kibongo ambaye ni kama alitushtua hv kwamba nasi tunaweza ishu hizi,anaitwa Steven Kanumba,naamini ni moja kati ya kazi za kitanzania ambazo hutakiwi kuzikosa aisii,sababu ziko kibao lakini mimi nakupa moja tu nzito ambayo sisi wadau wa haya mambo ya kuzitengeza hizi tunajua undani wake,ni kwamba imetengenezwa kwa muda mrefu(haijaripuliwa),nathubutu kusema imetumia mwaka mzima kutayarishwa mpaka kuletwa kwako,tofauti na zileeeeee za wiki mbili tayari eti unaambiwa iko dukani.Keshokutwa j5 pale club Billcanas inaoneshwa kwa mara ya kwanza(primiered).Ni Lovely Gamble itakayosambazwa na KAPICO TANZANIA Ltd.Usiikose.
MY DREAMS(MOVIE COVER)
Mzigo mwingine huu hapa wa "swahiba",unaitwa "My Dreams",huu utauona wiki hiihii kitaani kwako koz town nzima imeshachafuka na posters zake kali,umepigwa na RJ Company "vijana wa kazi"(sidhani hata kama huwa wanalala hawa jamaa) na unasambazwa na Steps Entertainment,nimeufuatilia sana mzigo huu katika hatua zote za utengenezwaji wake,naamini utakuwa NOMA sana,humo ndani macho yako yatamshuhudia Mahsein Awadh(Cheni),Rose Ndauka,Irene Uwoya(Mama Ndiku) na Vicent Kigosi(Ze dairekta),GRM wameshughulika,camera kabeba Razaq Ford na kwenye mashine "kaumiza mgongo"(editing) Ray mwenyewe,hebu fanyafanya kuutafuta.MY DREAMS.
DKT. MWIGULU AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA KITAIFA YA AFCON 2027.
-
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amekutana na Kamati ya Kitaifa ya
Maandalizi ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027) kwa ajili ya kupitia
hatua mba...





0 comments:
Post a Comment