LOVELY GAMBLE(MOVIE COVER)
Movie imetengenezwa na URBUN PULSE na imeshutiwa Uingereza,ndani kuna "galacha" wa filamu za kibongo ambaye ni kama alitushtua hv kwamba nasi tunaweza ishu hizi,anaitwa Steven Kanumba,naamini ni moja kati ya kazi za kitanzania ambazo hutakiwi kuzikosa aisii,sababu ziko kibao lakini mimi nakupa moja tu nzito ambayo sisi wadau wa haya mambo ya kuzitengeza hizi tunajua undani wake,ni kwamba imetengenezwa kwa muda mrefu(haijaripuliwa),nathubutu kusema imetumia mwaka mzima kutayarishwa mpaka kuletwa kwako,tofauti na zileeeeee za wiki mbili tayari eti unaambiwa iko dukani.Keshokutwa j5 pale club Billcanas inaoneshwa kwa mara ya kwanza(primiered).Ni Lovely Gamble itakayosambazwa na KAPICO TANZANIA Ltd.Usiikose.
MY DREAMS(MOVIE COVER)
Mzigo mwingine huu hapa wa "swahiba",unaitwa "My Dreams",huu utauona wiki hiihii kitaani kwako koz town nzima imeshachafuka na posters zake kali,umepigwa na RJ Company "vijana wa kazi"(sidhani hata kama huwa wanalala hawa jamaa) na unasambazwa na Steps Entertainment,nimeufuatilia sana mzigo huu katika hatua zote za utengenezwaji wake,naamini utakuwa NOMA sana,humo ndani macho yako yatamshuhudia Mahsein Awadh(Cheni),Rose Ndauka,Irene Uwoya(Mama Ndiku) na Vicent Kigosi(Ze dairekta),GRM wameshughulika,camera kabeba Razaq Ford na kwenye mashine "kaumiza mgongo"(editing) Ray mwenyewe,hebu fanyafanya kuutafuta.MY DREAMS.
SERIKALI YALIPA FIDIA YA SHILINGI MILIONI 999 KWA WANANCHI 103 WA DODOMA
KWA MIRADI YA MAJI
-
Mkazi wa Nzuguni, Benjamini Elias akisaini katika daftari la fidia wakati
wa zoezi la ulipaji fidia kwa wakazi wa Nzuguni jijini Dodoma ambao maeneo
yao...
0 comments:
Post a Comment