BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS

.......

.

Friday, April 16, 2010

MY ALBUM OF THIS WEEK(NEW AMERYKAH PT 2 by ERIKAH BADU)

Haya!haya!haya!haya tena wadau na fans wa blog ya burudani(muziki na maisha),its another "furahi-day"(friday) kama kawa najua utakuwa unahamu ya kutaka kujua leo nimekuletea albam ya nani katika ile "segment" yetu ambayo ilianza wiki iliyopita ya "My Album of the Week",kama nilivyokuahidi hii itakuwa ndio kama bye bye ya kukutakia weekend njema kabla ya "kufunga shule" kwa wiki hii si ndiooo???sema NDIOOO!!!Leo niko na mwanadafada mkali wa SOUL MUSIC na ambaye mtindo wake wa maisha umekuwa ukiwashangaza wengi,si mwingine niiiiiiiiiiii!!!!!ERIKAH BADU!!na albam yake mpya kabisa inaitwa "NEW AMERYKAH PT 2(the Return of ANKH).Hii ni albam ya saba na ambayo mwanadada huyo ameiachia kitaa rasmi 30 March mwa huuhuu kwahiyo bado iko moto kabisa.Lakini hii ni part II ya albam yake ingine aliyoiachia February 26 2008 chini ya lebo ya MOTOWN iliyoitwa "NEW AMERYKAH PT 1(4th World War).

NEW AMERYKAH PT 1
Mwanadada kajifungua mtoto mzuri wa kike Feb 1 mwaka huu na ilim'bidi kurudi home kwao BROOKLYN na mwezi wa tatu tu akaachia mzigo huu,mzigo una ngoma 12 zilizoshiba sana katika Soul na Hiphop Soul,vichwa vilivyopiga mzigo huo katika suala zima la production ni yeye mwenyewe pamoja na washkaji wengine kibao kama 9th Wonder,James Poyser,Shafik Huseyn wa SA-RA Creative Patners,Taarak,J Dilla,Madllib na Karriem Riggims.Ndani utasikia mikono mikali kama "20 feet tall","Window seat","Agitation","Get Money","Dont be Long","Love","Fallin in Love" na mingine kibao.Akizungumzia maana ya neno "ANKH" kama alivyolitumia kwenye albam yake hii(The Return of Ankh) Erikah Badu ametanabaisha kuwa "ankh" ni neno la kiarabu lenye maana ya "internal life" kwahiyo kiujumla amesema albam hii imebeba ujumbe wa "mvutano mkali wa kiimani na kihisia za ndani kabisa za mtu"(spritual and emotional battle).Na mzigo huu uko katika nafasi ya tisa kwenye BILLBOARD TOP 200 ALBUM CHAT.
NEW AMERYKAH PT 2
Boyfriend wake wa sasa anaitwa Jay Electronica na ambaye ndio baba wa mtoto wake aliyemzaa Feb mwaka huu,Erikah ana watoto watatu hivi sasa na kila mtoto ana baba yake,baba wa mtoto wake wa pili ni Big Boy aliyekuwa memba wa OUTCAST na ambaye walipata bahati ya kufunga ndoa na baadae kutalikiana.Huyu ndo ERIKAH BADU banaaaa so chekicheki hii albam ikuburudishe weekend yote hii halafu mimi na wewe tukutane hapa jumatatu au vipiiiiii!!!WEEKEND NJEMA FANS!!!!!!!!

NAHISI NINA MAKENGEZA(HEBU CHEKI NA HAWA JAMAA HAWAFANANI KWELI??)

JASON DELULO
CHRISS BROWN
Unajua mdau wangu kuna ishu zingine zinafurahisha sana,kila mtu ana kaugonjwa kake fulani hivi katika maisha ama mambo yake ya kila siku,sasa mimi mwenzio kaugonjwa kangu ni ka kufananisha watu,hata siku nikikuona wewe nitakufananisha tu pia teh!teh!teh!teh!.Wiki iliyopita nilikuletea picha mbili za jamaa ambao mimi nilikuwa nahisi wanafanana,alikuwa ni Justine Timberlake na Robin Thikle,nikapata comment moja toka kwa sister'angu mpendwa Yasinta,yeye akaniambia labda wanafanana pua tu,teh!teh!teh!teh!.Wengine walinitumia email wakinipa comments zao juu ya washkaji hao na kufanana kwao,thanx kwenu wote,sasa leo nakuletea hawa mabrotherman wawili,Jason Delulo na Chriss Brown eti wanafanana kweli?,kama vp cheki na video zao kwa makini halafu niambieeeeee!!!!poaaaaa!!!!

Thursday, April 15, 2010

MOSE RADIO&WEASEL TV WITH NEW ALBUM.

Mose Radio&Weasel Tv
Washkaji wanakula sana mashavu na si Kampala tu bali East Afrika na Ulimwenguni kote kwa ujumla.Kwa mfano mwezi May mwaka huu wana show ya kufa mtu Washington DC na mara nyingi wanamuziki toka East Afrika wakipata shows za mbele,juu kwa juu wanapata pia shows zaidi na zaidi na zaidi.Bebe Cool alikwishawahi kuwaponda hawa washkaji,akasema hawezi kutishika na watoto ambao hivi juzi kati alikuwa anawaona kwa macho yake mwenyewe wakiosha magari ya Jose Chamilion,lakini kiukweli mdau wangu tunapokuja kutazama ukali wa mwanamuziki au msanii fulani tunatazama kazi zake na wala si alichokuwa anafanya hapo kabla au sio??
Taaabaaasaaaam!!!!
Sasa sikia hii,washkaji wako tayari kurudi tena kwenu mashabiki na wanachoomba si kingine zaidi ya sapoti ya ukweli ambayo mmekuwa mkiionesha toka walipokuja kwa mara ya kwanza kabisa.Wanakuja na mzigo "mupyaaa" soon,baada ya "Nakudata" ambayo ni albam yao ya kwanza kabisa na "Nyambura" ambayo ilifuata,sasa mzigo mpya uko tayari kabisa,kinachosubiriwa ni kupakuliwa na hiyo itakuwa baada ya show yao ya May huko Washington DC.Sasa hivi vijana hawa wanafanya vizuri na "ability".Mimi nawasubiri,wewe???

HUYU NDO BANANA ZORRO BWANA!!

Banana Zorro
Kuna taarifa kuwa mwanamuziki(sio msanii) kutoka Tanzania na Rais wa bendi ya "kijasiriamali" The B-Band Banana Zahir Ally Zorro ana mpango wa kubadili aina ya muziki wake na kuanza kufanya muziki wa Rock and Roll,akizungumza hivi karibuni Banana amesema ameamua kubadili aina yake ya muziki ili kuwaletea ladha tofauti mashabiki wake na kufanya muziki anaoupenda zaidi,pia ametanabaisha kuwa muziki huo ndio uliomfunza kuimba wakati ule anasikiliza sana "kanda" alizokuwa nazo babake Mzee Zahir Zorro mwenyewe."Muziki huu ni mgumu sababu unahitaji skills za hali ya juu na vocos zenye nguvu,mimi nina kila kitu kwhy naamini hautanipa shida"amesema.Hebu tumsikilizie tuoneee!!!!!!

Wednesday, April 14, 2010

GUESS WHO IS THIS???

Nakuacha na hii,patishia huyu ni nani???halafu tuone kama kweli mdau wangu wewe ni kichwa.

SPECIAL KWA KIZAZI CHA BONGO FLEVA......

Vizazi vya Bongo Fleva ni ngumu sana kuyafahamu haya,na nimegundua kitu ambacho nataka ku-share nawe mdau wa blog hii ya burudani,hivi leo kuna baadhi ya ma'redio djs na watangazaji ambao wanajifanya wanaujua sana muziki huu wa KIZAZI KIPYA ,lakini kiukweli HAWAUJUI,nikijaribu kuwasikiliza kwa makini nagundua kuwa muziki wanaoujua ni muziki wa kuanzia miaka ya 2002 kuja mpaka hivi sasa,wanaujua muziki wa kuanzia enzi za hits za Bongo Records(P-Funk) kuja mpaka sasa,NIJUAVYO MIMI NI NGUMU KUKIJUA KITU VIZURI KAMA HUJUI KILIPOTOKEA,KILIPO NA KINAPOKWENDA,na huwezi kujua KILIPO na KINAPOKWENDA kama hujui kilipotokea.





                                                                                                                          
                            Kwanza Unity Foundation Makanga,ML Chriss(Blue)&Abbass(Yellow)

Hao hapo juu ni Kwanza Unity(K.U Crew),moja kati ya makundi waasisi wa muziki wenu huu ambao leo mnauita Bongo Fleva na ambao karibu kila mtu sasa anajifanya anaujua sana,kundi hili lilikuwa linaundwa na washkaji kibao tu kama akina K-Single(Kibacha),Easy B,Nigga One(RIP),Rhymson(Zavara),D-Rob(RIP),Fresh G na wengineo na walianza michakato hii mwishoni kabisa mwa miaka ya 80 mpaka mwanzoni mwa miaka ya 90 kipindi ambacho ndo "awamu ya kwanza" ya muziki huu wa kizazi kipya,kipindi ambacho tulikuwa tunaita "Swahili Rap".Na katika kipindi hiki ni makundi machache sana ndio yaliyokuwepo likiwamo hili la Kwanza Unity.Wengine walioweza kujitokeza katika awamu ya pili ambayo ilianza kwenye miaka ya 1994 ambapo muziki huu ulitambulika zaidi kama "BONGO HIPHOP ni  G.W.M toka pande za Kurasini,Diplomats toka Sinza,The Hard Blasters,Cycle Tack,Dar Young Mobb,W.W.A,Mawingu Band(walikuwa wanaimba),Bad Skins,Mack Muga(Solo artist),Erick aka E-Atack(Solo artist)Sos B(Solo artist),II Proud(Solo Artist),Ras Pompidou(Solo artist),Saleh Jabir toka Znz(Solo artist)Jotwa Jokeri toka Mwanza(Solo artist),WEPWAA toka Mwanza pia na wengine kibao ambao siwezi kuwataja wote hapa.
                                  Kwanza Unity Crew isipokuwa K-Singo na Samia X

Katika awamu hii ya kwanza ya muziki huu jamaa walifanikiwa kufanya albam moja "Kwanza Unity" ilokuwa na hit kama "amani" na zingine kibao tu,mwishoni mwa miaka ya 1994( awamu ya pili) ya muziki huu ambayo pia ndo ili-change jina kutoka "swahili rap" mpaka "Bongo Hiphop" ilikuja baada ya kuanza kwa vituo binafsi vya redio katika masafa mapya kwa wakati huo(masafa ya fm) na kidogo kuanza kutoa airtime ya nyimbo hizo wakati huo,Nakumbuka Radio One stereo(kipindi hicho ilikuwa 99.6fm now 89.5fm) ndo ilikuwa redio ya kwanza kwa hapa Dar na ilianza mwaka 1994 na kipindi cha kwanza cha vijana na kutoa airtime kwa nyimbo hizi kilikuwa ni Dj Show ya wakati huo na watangazaji walioanza kuzicheza nyimbo hizo ni Taji Liundi(Master T) na Mike Pesambili Mhagama.......

Mike Mhagama(kushoto) na Dj J4(kulia) 1997

Makala hii itaendelea wiki ijayo usikose....usikose kupitia blog ya burudani,comments zinahitajika..

Tuesday, April 13, 2010

HEBU SANUKA NA HII!!

Mr Matabane,George Zemdela&Mrs Matabane
Najua nitawastua watu kidogo koz hv sasa watu wamestukia sana tamthilia za ki-venezuela na ki-filipino,lakini hebu turudi kwetu Afrika kwanza,Isidingo(the need) tangu mwezi July 1998 iko hewani mpaka hii leo,ukiuliza watu watakwambia tumeichoka koz ni kama haiishi vile?Ila nataka nikwambie kitu kimoja umeshajaribu kuichungulia kidogo kwa sasa??ni noma mdau wangu,kinachonivutia now ni sakata la mtoto pekee aliyebaki baada ya mmoja kufariki(kitamthilia lakini) katika familia ya Matabane,Persons Matabane(Tshepo Maseko) kutokufanikiwa kumpa ujauzito mkewe mpya Thandi na Thandi kutaka apandikizwe mbegu za kiume za Mzee Matabane mwenyewe ili angalau azae mtoto ambaye atakuwa Matabane's,patamu hapo.
Persons&Thandi(ktk YOU Mag)
Tshepo Maseko ndo Persons katika tamthilia hii,na mmoja kati ya wakongwe wachache wa mwanzo kabisa katika ISIDINGO,alianza akiigiza kama mwanafunzi na amekuwa mpaka sasa ana familia yake na mkewe mpya Thandi baada ya kumtaliki mkewe wa kwanza Nandhipa.Jamaa alizaliwa 1978 Soweto S.A,baada ya kumaliza Kelokitso High School alijiunga na Pretoria Teknikon na kufanya diploma ya National Drama kwhy jamaa hajaungaunga kama wenzangu na mimi hapa Bongo.
 
Persons(Tshepo) with real wife
Mshikaji ni maarufu sana pande hizo na mbali na Isidingo ameshatokea katika tamthilia na tv shows kibao kama "Take 5","Badilammogo","A New Kind of Drawn","The Principle" na zingine nyingi.Pia sasa hivi ame-sign kama star wa docu-drama moja inaitwa "More than just a friend" ambayo itazungumzia ukuzwaji wa mpira wa miguu pande za Robben Island Prison.Hebu ichungulie ISIDINGO now hutaacha tena.....

NISAIDIE KAKA!!

Dj Choka.

Monday, April 12, 2010

MILAZO 101 YA MILLAD NEW SEASON ON MAY

Millad Ayo with Angelis
Show ni kali kwakweli na imepangika hasa,Milazo 101 ya Radio One na ambayo inafanywa na mtangazaji chipukizi na mkali Millad Ayo imesimama kidogo na itarudi rasmi katika season mpya kuanzia May mwaka huu,hii imekuja baada ya Millad mwenyewe kuwa likizo na show kukamatwa na Abdalah Mwaipaya kwa muda wa wiki tatu mfululizo,kwa sasa show ni non stop music kuanzia saa 10:30 mpaka 12:00 za jioni. 
Milazo 101 Logo.
Ninachoweza kusema ni kwamba fans wa Milazo 101 wataimiss sana show na tunaamini itarudi vizuri zaidi ya ilivyokuwa.Tunasubiri kwa hamu hiyo season mpya.Milazo 101 So fresh....So klean!!

ETI HEMED ANAKULA MARA 8 KWA SIKU,DUH!!

Hemed(Picha kwa hisani ya Ray The Greatest)
Inakuwaje wadau na fans??mko sawa??naamini weekend ilikuwa poa sana au vipi,its a brand'new week kama kawa kama dawa ni hapahapa katika blog yetu ya burudani tunakutana,tuanze na hii,wakati niko ndani ya gari najijongesha ofisini asubuhi ya leo nikainyaka hii,star wa muvi za kibongo na mwanamuziki wa R&B HEMED SULEIMAN eti anapenda sana kula,na huwa anaweza kula hata mara nane kwa siku,duh!!Hii imenistaajabisha na kunipa majibu ya maswali kibao ambayo nimekuwa nikijiuliza,kiukweli huyu jamaa nimemfahamu kipindi kirefu kdg hata kabla ya TPF-2 iliyomtoa,lakini kwa kipindi kifupi hivi karibuni amenenepa harakaharaka sana,kumbe sababu ni misosiiii alaaaaah!!Si mbaya but akumbuke kuwa yeye ni muigizaji so aki-overweight itakuwa ngumu sana kucheza baadhi ya sehemu katika muvi zinazohitaji wepesi kidogo kama kuruka ukuta ama uzio fulani,kukimbia sana na zinginezo,Hemed "kura ni kura rakini masoesi muhimu,sawa mura"??