BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS

.......

.

Wednesday, December 22, 2010

KIMYA KINGI??....MNM NEW SEASON COMIN' SOON 2011...

Naweza sema ilikuwa ni kipindi kirefi na kimya kirefu sana japo nilikuwa nadondosha vitu kimachalechale sana...but now fans wa MNM Blog kaeni tyr kwa msimu mpya wa 2011...kama kawa kama dawa wale woote ambao mlimiss ishuz kibao...kama ma-infoz na ishu ka hizo stay tuned..narudi upya kabisa na segments za hatari na infoz za kumwaga..hiyo ni katika msimu mpya wa Muziki Na Maisha Blog 2011..MNM "here we stay"....

Wednesday, December 15, 2010

TRUE LOVE IS HERE "CAMPAS CONNECT"...



Campus Connect” is the romantic late night radio show…aired on 106.5 Radio Mlimani of Dar es Salaam University @ 22;00pm-00;00am in every Mondays and WednesdaysShamimu Mlacha aka Shaney is the host of this show..”Campus Connect” talks about love and relationships, building love awareness to youths and adults, teach people how to behave in love and to forgive…”Campus Connect” is the place of comfort to broken hearted people…slow jams, soul music & all good music here is the place to be…This is ”Campus Connect”…we believe in TRUE LOVE.Lets be there!!For anything please use contacts below….Don't u ever miss this show...



Contacts;


Email;shamimumlacha@yahoo.com


www.facebook.com/campasconnect

Thursday, November 25, 2010

HAPPY BIRTHDAY MY GOOD FRIEND ISSABELAH WA V-fm

ISABELLAH NSHAMA

Leo tar 25 Nov ni siku nzuri na ya furaha kwa rafiki yangu wa ukweli...Isabellah Nshama wa Victoria fm ya mjini Musoma..wengi walitamani wafikie umri ulionao wewe but ilishindikana..hongera sana na MNM inakutakia birthday njema..we wish u to blow a lot of candles one day...Happy Birthday Isabellah..

Friday, November 19, 2010

IN THE MAKING OF THE MOVIE...(JINA KAPUNI).....PT I










HAPPY BIRTHDAY MY YOUNG SIS NEMY NIQY..

NEEMA KILUVIA aka NEMY NIQY

Leo Nov 19 ni siku muhimu sana kwa familia ya Mr&Mrs Kiluvia,coz kitinda mimba aka mziwanda aka lastborn Neema Kiluvia aka Nemy Niqy anakumbukia siku yake ya kuzaliwa..mimi kama brother na kwa niaba ya wana familia wote..namtakia birthday njema,Mungu amsaidie atimize yale yote anayoota kila siku...Happybirthday Ney..

Saturday, November 13, 2010

Monday, November 8, 2010

MBEYA...KAZI IMEANZA..NI EBONY FM PEKEE...

Ki-historia ni muziki ambao inasemekana haujawahi kutokea..but Ebony fm imebadili kabisa hali ya hewa ya burudani jijini Mbeya...MTIKISIKO 2010 "bata mreeefffffffff" sana ameliwa Mbeya jumamosi ya wiki iliyopita..ilikuwa ni noma..kwa udhamini wa VodaCom Tanzania,Kilimanjaro Premium Lager na PSI Tanzania...tazama down hapa>>>>

Muonekano wa stage wakati ikifungwa mchana...ni Ebony Entertainment banaaaa.......


Na hii ni namna ambavyo stage ilikuja kuonekana usiku mnene kwenye bataaaa....


Akhsanteni Mbeya kwa kutusapoti....here we are na burudani zitakuja zaidi na zaidi na zaidi


Visigino vya Twanga vilisuguliwa kama kawa...Twanga Pepeta on stage..


Linah kutoka THT..akiwakilisha kama kawa kama dawa pale kati..


Juma Kassim Kiroboto aka Juma Nature..mmoja kati ya wasanii wasiochuja hata kama hana ngoma mpya redioni..huu ndio ulikuwa moto wake..."msichana mtundu,msichana mtundu,msichana mtundu.".



Dj Mubba "the proffessional" on the wheel of steel...schrachings!!
Sasa mpango mzima ni Jmosi hii Iringa town katika viwanja vya Samora...MTIKISIKO 2010.."bata mreeeeeeffffff" tutaendelea kumla pale..usiikose..

Friday, October 29, 2010

EBONY FM..HERE WE COME AGAIN..MTIKISIKO 2010.

STAGE ON CONSTRACTION

Mwaka wa nne now...tamasha lilianza since 1997...Bigtime Highland Company Ltd na Ebony Entertainment....kupitia d' hottest radio stations never appeard on Earth...Ebony fm n' Hot 89.5fm..wanadondosha only a single but rememberable East African Music Festival day...almaaruf "MTIKISIKO"..its once upon a year...na mwaka huu ni MBEYA & IRINGA regions...this year it goes with the slogan "bata mrefffff!!!"...Artistslist ni ndefu balaa...but special appearance ni ma'men WEASEL&RADIO from Kampala n' one&only sexy lady all the way from Naiii...called herself WAHU...hii ni kwa uchache tu..sticky around with MNM for more info....

WAHUU WITH HUSBAND NAMELESS

Tuesday, October 26, 2010

BAADA YA JADEN....NOW SMITH'S FAMILY PRESENTS...WILLOW SMITH..

WILLOW SMITH

Hii ni baada ya familia kumsapot na kufanikiwa kumtoa first born wa Jada Pinket Smith...Jaden Smith katika movie Karate Kid now Smith's family inamtambulisha kwenu last born wa Will Smith...Willow Smith..lakini sasa sio katika movie tena..ni katika muziki...jana nimebahatika kutazama 106&Pack na Willow alikuwa anatambulisha singo yake ya kwanza "Whip My Hair"...ni bongebonge moja la track...ni njia nzuri kwake na ni dalili za kuja kuwa moto ile mbaya..sasa je wazazi wa kitanzania twajifunza nini kutoka Smith's family???

SMITH'S FAMILY WAKIINGIA KWENYE STUDIO ZA BET

PIGO JINGINE IN REGGAE MUSIC...GREGORY ISAACS HAS GONE FOR GOOD...

GREGORY ISAACS

Ni kifo cha Jamaican Reggae Icon Gregory Isaacs kilichotokea jana asubuhi nyumbani kwake London Uingereza..baada ya kuugua kwa muda mrefu sana ugonjwa wa ini kushindwa kufanya kazi..Meneja wake Copeland Forbes amethibitisha kutokea kwa kifo hicho...amefariki akiwa na miaka 59..alizaliwa July 15 1951 huko Fletcher's Land Kingstone Jamaica na alianza rasmi kurekodi mwaka 1960...na ndipo kabla ya mwaka 1970 akachomoza na hit kali zilizomtambulisha kama "Love is Overdue" na "All I have is Love"....mimi nilimtambua zaidi katika "Night Nurse"...MUNGU ailaze roho ya marehemu Gregory Isaacs mahali pema peponi..Aamin!!

Tuesday, October 12, 2010

ZINANIKUMBUSHA MBALI...."BROWN SUGAR" BY D' ANGELO..

"BROWN SUGAR"

Released July 3, 1995

Recorded 1994–1995
Battery Studios, RPM Studios
(New York, New York)
Pookie Lab
(Sacramento, California)
Genre R&B, neo soul, soul, funk
Length 53:17
Label EMI
Producer D'Angelo, Kedar Massenburg (exec.), Ali Shaheed Muhammad, Bob Power, Raphael Saadiq
D'Angelo chronology
Brown Sugar
(1995) Voodoo
(2000)
Singles from Voodoo
1."Brown Sugar"
Released: August 1, 1995
2."Cruisin'"
Released: October 12, 1995
3."Lady"
Released: February 20, 1996
4."Me and Those Dreamin' Eyes of Mine

ALI KIBA HUYOOO...INTERNATIONALY...

ALI KIBA

Awali nilipopata taarifa kuwa Ali Kiba ameachana na management ya awali chini ya G-Records ya mtu mzima Gulu aka G lover nilihuzunika sana...na nikaona sasa kijana amepotea na muda si mrefu tutamsahau...aisiii..i was wrong...very wrong bana...kijana juzi kati ame-sign na kampuni ya kimataifa ya "RockStar4000" yenye uhusiano na Sony BMG ya nchini Marekani na soon ataanza kusikika kimataifa zaidi...kazi ya kwanza ya kampuni hiyo kwa Kiba ni kusambaza nyimbo zake za albam zake mbili za kwanza kimataifa zaidi... na mengine tutajulishwa...hii ni akili jamani au sio??kila la kheri mwana!!

RAY&KANUMBA IN THE BATTLE ONCE AGAIN....

"PRETTY GIRL"(COVER)

Hii ni mara ya pili kwa wasambazaji wakubwa wa filamu za kibongo kampuni ya Steps Entertainment kulifanya hili....kuingiza sokoni kwa wakati mmoja filamu mbili za magwiji wa filamu nchini...Ray Kigosi na Stiven Kanumba...na ile ya kwanza niliiripoti hapa pia..sijui matokeo yalikuwaje kibiashara nadhani Steps wenyewe wanalo jibu...sasa this time ni "Pretty Girl" toka RJ Company na "Uncle JJ" toka Kanumba TheGreat Films...zote kwa wakati mmoja zitakuwa sokoni time yoyote kuanzia sasa...tuone tena "Nani ni Nani"..

Thursday, October 7, 2010

MAONI YA MDAU TAJI LIUNDI BAADA YA "BLACK SUNDAY" PREMIER..

BLACK SUNDAY(COVER)


Nilipewa DVD ya kuangalia kabla ya filamu kuzinduliwa na watengenezaji nikiwa ni rafiki na mshirika wao katika mambo kadhaa.
Nilisikitika mara tu nilipoanza na kujikuta naangalia filamu ambayo dhahiri ilik...uwa imeigwa. Kadri filamu ilivyoendelea, nilishtushwa na hadithi, maudhui na hata tamati. Vyote kwa sehemu kubwa vilitokana na filamu ya mwaka 2007 iliyotengenezwa Canada inaitwa BUTTERFLY ON A WHEEL.
(ANGALIENI PROFILE WALL KUONA TRAILER ZA FILAMU HIZI MBILI)
BUTTERFLY ON A WHEEL ni sawa na kusema KIPEPEO KWENYE GURUDUMU. Kama kweli unataka kumkanyaga kipepeo, basi gurudumu ni kitu kikubwa sana. Mantiki ni jina hilo ni sawa na kusema kwamba, 'jitihada kubwa mno inatumika kutimiza swala dogo sana"
Ndivyo zilivyo hadithi zote mbili. Mtekaji anatumia mbinu na kila jitihada kuwabughudhi wapenzi wawili kutwa, kwa sababu ambayo inabainika kuwa ndogo lakini nyeti. Ukosefu wa uaminifu katika ndoa.
Black Sunday ina mapungufu mengi sana.Imeigwa.
Haina uhalisia, hata kama ni filamu ya kubuni. Kanumba kwa mfano anaonyesha bastola waziwazi, anawapa wahanga wake nafasi nyingi za kutoroka na labda kubuni mbinu za kumzidi.
Haiwezekani kutoa Shilingi 50+milioni siku ya Jumapili bila benki yeyote (Pilipili Bank?) kutaka kujua kwanini au kukudadisi kwa undani?i!Jinsi ya mtoto katika filamu inajichanganya!Mara binti, mara mvulana???
PLOT: haina nguvu, si ajabu kwani imeigwa na kuleta uhalisia wa Tanzania iliwashinda waandaaji.
Mf.Mlela na Yvonne hawana hata sumni mfukoni, lakini wanapotumwa kuombaomba hela, wanaonekana kufika hadi MJINI kutoka Giraffe Ocean View Hotel! Labda Mrwanda hataelewa sawa...
Uigizaji wa Kanumba sio mzuri. Anavituko vya "kitoto' sijui niseme? Kugonganisha meno, kula Big G na kuifanya iwe kama kitu cha msingi sana. Kiujumla SCRIPT yake ni mbaya. Hasemi lolote la maana kwa robo tatu ya filamu.Kuna umihimu wa kukubali STRONG CHARACTERS siku nyingine.
Mlela na Yvonne hawapati nafasi ya kuzungumza wala kuigiza haswa kwa zaidi ya robo tatu ya filamu nzima.Hata hivyo, filamu inaisha na matukio ya kushangaza akili za mtu mwerevu!
Hakuna utaalamu wa taa, SPECIAL EFFECTS, na LOCATION au utafutaji wa maeneo ulikuwa finyu sana!
Sijaelewa waandaaji wanawaza nini? Sifahamu kama waigizaji walifahamu kwamba walikua wanatoa kopi. Hawajajibu maswali yangu niliyotuma kabla ya kuandika haya.
Nashindwa kuzipenda sana kazi za nyumbani. Umakini, ubunifu na utungaji hadithi zenye kina unatuangusha.
Kitu kizito zaidi ni SOKO. Mlimani pale wanaenda watu wa tabaka la juu kuangalia kwa mfano INCEPTION. Matarajio yao ni kuangalia filamu za kiwango cha juu sana. Wanaweza kila wiki kuingia kuangalia filamu kwa Tsh 8.000-15 elfu!Kama panajiendesha na soko hilo tu peke yake, je kama rafiki yangu Kanumba angeweza kujitahidi kufikia viwango vya kukubalika na soko hili? Si angefaidika sana?
Soko la KWELI sio la VIDEO ni la MAJUMBA YA CINEMA. Uuuzaji wa video ni BAADAYE kabisa.Lakini hili ni somo la siku nyingine...Haya, nimenena. Ni matarajoio yangu kwamba wengi mtaona nimekuwa mkali kwenye maoni. Nimekuwa mkweli. Kama hukwenda kuiona, ione kwanza au inunue kisha pitia upya niliyoandika. Kwa wasanii husika, msinichukie, msichukie niliyoandika, hebu chukulieni maneno haya kwa fikra chanya.Naamini sisi ni marafiki na rafiki mwema ni yule ambaye haogopi kusema ukweli. Ukweli unauma. Ukweli unajenga.Naandika kuwafumbua macho na kuwatakia maendeleo. Hakuna fani yenye kukosolewa zaidi kama FILAMU. Nipo tayari kuendelea kushirikiana nanyi katika mawazo. Natumaini waungwana wengine wataandika maoni yao nao.
Kila la kheri.
TajiSee More


Tuesday at 2:02pm · LikeUnlike

Tuesday, October 5, 2010

TONIGHT ON 106 & PACK @ BET...JEREMIAH IN THE BUILDING...

JEREMIAH

Leo usiku kwenye 106 & Pack ya BET...bongebonge moja la interview la mtu mzima Jeremiah...so kama vp cheki mida ya saa tatu kamili usiku kwa saa za kibongo...

BET HIPHOP AWARDS 2010...NICKI MINAJ STILL SHINING..

NICKI MINAJ(BET HIPHOP AWARDS 2010)

Ishu ilikuwa juzi tu Oct mbili huko Atlanta...ni tuzo za maalum za Hiphop za BET(Black Entertainment Tv) 2010....Jay Z na Nicki Minaj wamesemekana ku-shine ile mbaya baada ya kuzoa tunzo kibao...sasa hapa down tazama washindi kwa ujumla....


*MVP of the yearDrake


*Best Video
Jay-Z and Alicia Keys for “Empire State of Mind”
*Favorite By Fans
Nicki Minaj
*I Am Hip-Hop Award
Salt-N-Pepa
*Rookie of the Year
Nicki Minaj
*Made You Look Style Award
Nicki Minaj
*Perfect Combo Award
Jay-Z and Alicia Keys for “Empire State of Mind”
*Track of the Year(Producer of the year)
Lex Lugar for producing the track “B.M.F.”

Friday, October 1, 2010

YOUNG DEE ON "TUPO PAMOJA SHOW" THIS FRIDAY..

ARNIE GIZZLE

..............."naitwa Arnie Gizzle........Unataka kujua leo nipo na nani humu ndani?"........... Ni moja ya maneno niliyokuwa najaribu kuzungumza kipindi nafungua show. Hapo kati nimeshatupia vitu zangu kutoka FELIX SINZA CLASSIC WEAR haajah jaah jaah!! nang'aa kama... Nway karibu katika show!!!!!!!!



YOUNG DEE

Namwita bwana mdogo kiumri but mkubwa kwa jina, Anaitwa Young Dee!!! Hapa Gizzle na Crew ya Tupo Pamoja ilifanya kumtilia maguu kitaa na kuchonga nae Machache kuhusiana na Muziki wake na nini anafanya kwa sasa na pia tutegemee nini kutoka kwake?.....



ARNIE GIZZLE&YOUNG DEE


Unakumbuka ngoma ya Teacher?? iliyopikwa pale kati FishCrab na mtu mzima Lamar... This time Young Dee anakuja na project mpya kutoka Studio ya ukweli pale AUTHENTIC kwa mtu mzima MAX..... Daaaaah humo ndani kuna ngoma moja kali sana inaitwa KIATU....Daaah fanya kutazama show this Friday uwe wa kwanza kuisikiliza haaaaaa haaaaah!!!!!!



MAX

Huyu ndio Max wa AUTHENTIC ... Jamaa ni mkali wa sound na Ideas kibao , zaidi ndio mtu anayempa training Young Dee kwa sasa pale kati... Pia ni msaani anayeimba ...... na anazo ngoma kibao na moja ya ngoma zitakazo make headline ni One Minute ambayo kafanya Collabo na Young Dee.... Fanya kucheck show afuu tuoneeeeeeeeee!!!!!!



ERASTO MASHINE

Huyu ni mchawi wa Beat anaitwa Erasto Mashine... Anapatikana pale kati AUTHENTIC ndio anafanya mambo yote mle ndani pia ndio mpishi wa track mpya ya Dee Inayotegemea kutoka hivi karibuni...... Unataka kumjua anafanyaje??? Don't miss the show @9pm this Friday Only on Ttv.









Thursday, September 30, 2010

COMING SOON..."LOUD" BY RIHANNA..

LOUD(ALBUM COVER)

Kafanya poa ile mbaya na mzigo uliopita unaitwa "Rated R"..sasa mwanadada anatua mzigo mwingine Nov 12 mwaka huu ambao karibu kila mtu anasubiri kuona itakuwaje??mzigo waitwa "LOUD"....ungojee....

TOMMOROW NI "SUPER FRIDAY" ON THE PEOPLES STATION


Kesho ni "Super Friday" ndani ya Clouds fm "redio ya watu",na hiyo ni katika kusheherekea kitofauti hati ya kuwa super brand radio station iliyotunukiwa na kampuni ya Super Brand International ya nchini Uingereza...so ijumaa ya kesho itakuwa ni ijumaa maalum kabisa kwa redio hiyo kukumbuka ilikotoka kwa kuwaalika na kufanya vipindi walivyokuwa wanafanya wakati wa "struggle" baadhi ya watangazaji  na madj waliowahi kupiga mzigo hapo(wengine bado wapo ila wanafanya shughuli zingine)...baadhi yao ni kama Terrence, Taji Liundi, Ray C, Judith Wambura(JayDee), Fina Mango, Seven, Bobby, ML Chriss, Boggie Master, Jimmy Kabwe, Sakina Lioka, Dj Bonnie Lov, Dj Venture, Dj Mully B, Mr D, Mr C na wengineo ambao wataweza kupatikana...kwa habari kutoka ndani kabisa ya kituo hicho zinasema kesho itakuwa ni siku ya kukumbukwa na ni siku ambayo hakuna msikilizaji atakayetakiwa kuikosa...ni "Super Friday" On the peoples station...

Wednesday, September 29, 2010

UJUMBE WA SKYWOKA KHS HALI YA KIDBWOY...

SKYWOKA

Nilikuwa facebook muda si mrefu nikakutana na ujumbe huu toka kwa SkyWoka..mshkaji na mtu wa karibu zaidi na KidBwoy kwenda kwa fans na friends wote....
"Kwa marafiki zangu wote> Hali ya Kid inaendelea vzr sasa hv. Jana jioni nilienda kumchek nilimkuta amelala. Mama yake alinambia karibu kila mtu anamkumbuka sasa hv na mara nyingi anakuwa na hamu sana ya kuongea lakini kutokana na maumivu ya kichwa haruhisiwi kuongea sana. Ameambiwa ana hitaji utulivu wa hali ya juu. Kwahiyo jamani kwa sasa hatuna tena wasiwasi mkubwa juu ya afya yake. Thnks"
From MNM...
Thanx man Sky...twazidisha maombi ili mshkaji awe fresh soon..na twashukuru pia kwa updates za hali ya Kid pia coz we r so much inlove kwa mshkaji na kwa bht mbaya tuko mbali so inakuwa ngumu kumtembelea ili kujua hali yake...MUNGU NI WETU SOTE...ATATUSAIDIA...ONELOVE!!

Tuesday, September 28, 2010

HONGERENI KWA KUWA "SUPER BRANDY"....CLOUDS FM

Siku zote maisha ni safari ndefu..na mvumilivu hula mbivu...ni safari ngumu ya MAFANIKIO kwa miaka kumi sasa..hongereni kwa kutunukiwa nembo ya SUPER BRANDY fm station..kwenu CLOUDS fm(People's Station)...


Toka enzi hizi...si mchezo manake..ilikuwa ndoto inaotwa ...



Zikaja enzi hizi wkt ambapo ndoto imekuwa kweli...timu ya awali kabisa ya 88.4 Clouds fm(1999)



And now....guess wat???bata!bata!bata mjini...safari na mafanikio kibao ya mpaka leo kuwa Super Brandy fm station only in Tanzania...hii ni sehemu ndogo tu ya timu kubwa ya Clouds Media wakiwa na mwanaharakati Shy-Rose Banji.

Thursday, September 23, 2010

HAYAWI HAYAWI SASA.....KIBOKO CHA ORIGINAL KOMEDI HIKI HAPA...LEO USK

ZE COMEDY SHOW

Leo pale kati show hii inaanza..kupitia "The # 1 youth channel" EATV..washkaji wamesota sana..kwa muda ambao ungekuwa wewe ungeshakata tamaa..ila kuanzia leo ni bata tu coz show ndo itakuwa kwa hewa..tusubiri tuone kama je ni kiboko kweli cha Original Komedi waliokuwa hapa na sasa bata zinaliwa TBC 1??Jibu unalo wewe mwenyewe...

COMING SOON..."PINK FRIDAY" BY NICKI MINAJ

"PINK FRIDAY"(COVER)

Baada ya kugonga copies kibao na mzigo wa kwanza "Massive Attarch"....Nicki Minaj toka lebel ya Young Money sasa anashusha mzigo mwingine matata sana "Pink Friday"...Huu ni mzigo wake mpya kabisa ambao mpaka sasa bado hajatambulisha mkono hata mmoja toka humo ndani...ni juzi tu ndo ametamka rasmi jina la mzigo wenyewe na kutambulisha official cover(kama unavyoona)..Mzigo utadondoka kitaa rasmi Nov 23 mwaka huu..nausubiri ile mbaya..

KIDBWOY AENDELEA VZR..AHAMISHWA WODI..

KIDBWOY

Wadau na fans wengi walitaka kujua mchizi anaendeleaje..baada ya kuripotiwa kuvamiwa na kuumizwa vibaya na mtu asiyefahamika anayesadikiwa kuwa ni msanii....Mtayarishaji wa muziki na mmiliki wa TETEMESHA Records ambaye pia ni mtangazaji wa Radio Free Africa ya Mwanza Sandu George Mpanda al-maarufu kama KidBwoy kwa sasa hali yake inaendelea vzr..ameweza kuzinduka na kuzungumza japo kidogo baada ya kuwa nusu kaputi kwa zaidi ya masaa 15 baada ya tukio...ila habari mpya zinasema mshkaji imebidi ahamishwe wodi ili kuhepuka usumbufu wa fans kibao ambao daily walikuwa wanajitokeza hospitali ya Bugando alikolazwa kwa nia ya kumjulia hali na kutaka kupigapiga nae stori ishu ambayo madaktari wake wamesema si salama sana kwa sasa coz anahitaji mapumziko zaidi...awali alikuwa wodi no C 606 ghorofa ya sita...kwa sasa amehamishiwa wodi ambayo bado haijawekwa wazi ili apate mapumziko na kuharakisha kupona kwake...Get Well Soon Kid.

HAPPY B'DAY JERMAIN DUPRI...

JERMAIN DUPRI

Mdau leo tar 23 Sept ni siku ya kuzaliwa kwa mmoja kati ya watayarishaji wakali nnaowaaminia wa muziki nchini Marekani Jermain Dupri...so mchizi anasheherekea siku yake leo..kama nawe ni B'day yako leo fahamu kuwa unashea b'day na star huyu...Happy B'day Jermain Dupri..

Tuesday, September 21, 2010

OLD SKOOL....."H-TOWN"...

H-TOWN