BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS

.......

.

Thursday, January 20, 2011

STARTING TOMORROW..MY NEW SEGMENT IN "VUTA PUMZI" SHOW ON EBONY FM


Ni dakika chache sana kwa kuzifikiria kikawaida kichwani..but ni nzito na muhimu sana kwa ajili ya kuifungua weekend yako...ni segment yangu mpya itakayoanza ijumaa ya kesho na kila ijumaa ndani ya "Vuta Pumzi" show..si pengine ni EBONY fm (87.8..Iringa, 88.2..Moro&Dom na 94.7..Mbeya).."KIJA'S 15" ni live from Dar es Salaam Tanzania na hutakiwi kuikosa...bila hii bado hujaanza Weekend,itakuwa na nini ndani??bado ni surprize!!!

Tuesday, January 18, 2011

IN R&B THANG....CHICO DEBARGE!!


Jina halisi ni Jonathan Athur..ambaye alizaliwa June 23 1966 Detroit Michigan US..ni mdogo wake na mmoja kati ya memba wa Motown Family Act Debarge...alianza kuimba miaka ya 80's akiwa chini ya Motown  na albam yake ya kwanza "Chico Debarge"
 ilibeba hit "Talk to Me"..hii ilitoka 1986...baada ya hapo ikafuata album ya pili "Kiss Serious" mwaka 1988...bahati mbaya akafungwa jela kutoka na dili za dawa za kulevya..akapotea kimuziki na akaachiwa katikati ya miaka ya 90's...



 Akarudi Motown na akafanya albam "Long Time No See" mwaka 1997 ikafuata "The Game" mwaka 1999 na hakukaa sana akaondoka na kuhama lebel...akahamia Koch Records ambapo akaachia mzigo "2003's Free"...album ya sasa inaitwa "Addiction" ambayo aliiachia July 14 2009 chini ya Kedar Entertainment Group...mchizi ana watoto watano na tyr amekwisha mpa talaka mkewe aliyemzalia watoto wanne coz mtoto wa tano alizaa na mwanamuziki na muigizaji Nona Gaye.Its R&B Thang!!Kazi imeanza!!

MULT-TALENTED DUDE..SKY WOKA WE NI NOUMER..


Nafahamu kwamba b4 hajaingia ktk utangazaji alikuwa mmoja kati ya ma-MC wanaoogopeka sana Musoma town pale..but baada ya kuingia katika utangazaji ikawa kama imesahaulika vile..naona sasa anarudi mdogomdogo coz mara ya mwisho nilimsikia akichana katika track ya kwanza kbs ambayo huwa haitajwi(sijui ni kwanini) ya Hussein Machozi "Samahani" aliyoifanya pale Tetemesha na mikono ya Kid ikahusika sana...baadae nikaja nikasikia bonge bonge moja la track yake mwenyewe aliyofanya na Farida "Ree Kay"(sijui iliishia wapi ile) pale pale Tetemesha...Anaitwa Fredrick Bundala aka Sky Woka..sasa ana mikono miwili mikali sana..kinachonivutia ni namna anavyofanya muziki wake...mfano hii ya sasa swahili version ya "Am coming Home" ya Diddy Dirty Money" ni noumer..Sky we ni mkali sana...but naomba uendelee kufanya muziki huohuo unaoufanya sasa..don't change man.

Monday, January 17, 2011

ITS MY BIRTHDAY....NA KAZI NDO INAANZA 4 2011..


Ni kitambo kirefu najua mlinimiss ile mbaya...mlimiss vitu ambavyo naamini katika kipindi chote ambacho sikuwa hapa mmeshindwa kuvipata sehemu nyingine yopyote...na ndo maana nimekuwa nikishuhudia IDADI ya wahudhuriaji ikiongezeka japo sikuwa natupia chochote hapa...KIUKWELI mmenipa MOYO sana na nimeamini ninyi ni funs wa UKWELI sana kwangu na MNM kwa ujumla..THANX SO MUCH...sina cha kuwalipa kwa namna yoyote tofauti na kurudi kwa NGUVU zote kuwapa kile mlichokimis...am HERE NOW..nipokeeni jamani...leo ikiwa ni SIKU yangu ya KUZALIWA naitumia kukupeni taarifa kuwa now MNM is alive..tuendeleeni kupashana hili na lile...infos hapa ndo mahali pake..4 anything check nami katika mail yetu ileile bizzo4shizzo@ymail.com....au inbox me kwenye facebook...www.facebook.com/renatuskiluvia...au kiurahisi gonga pale palipoandikwa "niko huku pia" pembezoni mwa blog hii...THANX!!

BEST COMEDIAN FOR 2010..ATHMAN MWALUBADU..


Ni mchizi wangu na workmate wangu pia...nami huwa nikikutana nae tu naanza kupasuka mbavu kabla hata hajaongea wala kusema chochote..nilijua huku atafika..anaitwa Athman Musa Mwalubadu..mchekeshaji na mtangazaji wa Ebony fm(the no oneRadio Station in Southern Highland )...ambaye juzi kati amenyaka tuzo ya mchekeshaji bora wa mwaka 2010 toka Film Central Awards ambazo zilitolewa na mtandao maalum wa kutangaza kazi za filamu hapa Tanzania ujulikanao kama filmscentral.co.tz....na hii imempatia tunzo Mwalubadu ambaye hajashiriki comedies nyingi kivile sana kama wachekeshaji wengine tunaowaona kila siku...Big Up Bro...naamini safari bado INASONGA..na wataisoma namba au sio???