BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS

.......

.

Friday, September 3, 2010

7 YEARZ AGO..SENGEREMA MWANZA..(CHOKA MBAYA RECORDS)

DAW MAJUKANO&RENATUS KILUVIA

Nimeona sio vibaya nikishea nanyi fans wangu..asb ya leo nimepokea simu toka kwa mshkaji wng wa ukweli sana Daw Majukano na kunipa taarifa zilizonishangaza sana...eti blog tuliyoifungua miaka nane iliyopita bado iko hewani mpk leo hii..duh!!Kweli bana..nilipoi-google nikafanikiwa kuifungua na kuiona...aisiii!!kiukweli nimekumbuka mbali sana mdau..hii ilikuwa ni blog ya kuitangaza studio yetu ya kwanza kabisa "Choka Mbaya Records" ambayo tuliifungua na kuanza kufanya kazi ya recording mwaka 2002 Sengerema Mwanza wkt huo tukiwa watangazaji wa kituo cha redio 98.8 fm cha wilayani humo...baadae tulihamisha studio jijini Mwanza na kubadili jina toka Choka Mbaya na kuwa Stonetown Records, halafu Zanzibar(Stonetown I) na Shinyanga(Stonetown II) na mwisho zikaungana mwaka 2007 Kinondoni Dar es Salaam.

STONETOWN RECORDS

Ni safari ndefu ambayo sitakaa niisahau kamwe katika maisha...hapa chini nakuwekea baadhi ya posts tulizoweka kujitambulisha ktk blog hiyo....
"Maelezo kidogo kuhusiana na Studio za CHOKAMBAYA

Choka mbaya records ilibuniwa mwaka 2000. lakini ilianzishwa rasmi mwaka 2003--- december chini ya ma-deejayz wawili ambao ni David james majukano. a.k.a deejay daw na mwenzie Renatus Albinus kiluvia a.k.a rennie bizzo wote wakazi wa jijini Mwanza Tanzania East afrika.CHOKAMBAYA RECORDS ni Studio ya kurekodi muziki aina zote. Neno "chokambaya" linamaanisha kuchoka vibaya( so tired records) hehehehehehe!!! alisema rennie bizzo!! nia na madhumuni ya kuanzisha STUDIO hii na kuisimika jijini mwanza ni kuinua vipaji vya;WASANII chipukuzi wa muziki mbalimbali. kama..HIP-HOP,R&b;b,ZOUK, REGGAE NYIMBO ZA DINI;NYIMBO ZA KITAMADUNI (TRDITIONAL; MUSIC) NK!!! CHOKA MABYA RECORDS ni Studio pekee iliyoko maeneo ya Sengerema na inawakilisha maeneo mbalimbali kwa mfano Geita, mpaka Ngara !!! Dee-jay Daw ni mtangazaji wa radio vilevile ni "PRODUCER" wa "CHOKAMBAYA RECORDS" Rennie Bizzo nae ni mtangazaji na pia ni PRODUCER" ndani ya "CHOKAMBAYA RECORDS"
                      
                    WASANII WOTE MNAKARIBISHWA!!


"Kama wewe ni msanii wa maigizo,muziki wa aina yoyote basi kuwa huru kuwasiliana na sisi .kwa msanii anae toka mbali kidogo na maeneo ya sengerema yaani kwa mfano mwanza city kuja kwetu kurecord atarudishiwa ghalama zake za usafiri na huwa tunawapa kipau mbele sana wansanii kutoka mbali"

Link yenyewe ni http://www.chokambayarecords.8m.com/

Thursday, September 2, 2010

MKOLONI WA WAGOSI KTK HALI TETE...

DK JOHN NA MKOLONI

Mdau na fan wangu,hii nimeinasa hivi punde japo imewekwa kitambo kama cha masaa 19 yaliyopita katika Facebook na mwandishi wa habari za burudani toka Mwananchi Communication na mtangazaji wa kipindi kipya cha "kituo cha kazi" 100.5 Times fm Henry Mdimu..imesomeka kama hivi..
"BREAKING NEWS: Mshkaji wetu Fred Mariki, a.k.a Mkoloni wa kundi la wagosi wa Kaya, ambaye ni producer wa kipindi cha kituo cha kazi, amezimika baada ya kunywa supu inayodaiwa kuwa na madawa, na amekimbizwa hospitali ya Mwananyamala ambako amepumzishwa, tusaidiane kumuombea ili arudi katika uzima wake,na mambo yawe hewani kama kawaida..."
Hii imetokea Meeda BAR Sinza,tuungane pamoja tumuombee arejee barabarani soon.

MABIBI NA MABWANA..NAMLETA KWENU..JANE MISO.

JANE MISO


Baada ya kutamba na album yake ya kwanza "OMOYO" aliyoimba kwa lugha ya kisukuma ktk baadhi ya nyimbo, sasa anakaribia kupakua "UINULIWE" yenye nyimbo maalumu za kuuombea uchaguzi mkuu wa Oct 31 mwaka huu,ambao awali alipanga kuizindua albam yake aliyokuwa akiitengeneza kwa muda mrefu "MOTEMA" yenye mahadhi ya Lingala yenye nyimbo sita ambayo sasa itazinduliwa wakati mwingine. Kwa sasa yuko tayari kuileta kwenu (audio na video) "UINULIWE" Sept 19 katika ukumbi wa Diamond Jubilee na maandalizi yote yamekwisha kamilika ambapo ataisambaza punde atakapomaliza uzinduzi huo ambao pia utapambwa na wahudumu wengine wengi kutoka ndani na nje ya nchi.

Wednesday, September 1, 2010

DIDDY AKUBALI MATOKEO......

SEAN PUFFY COMBS

Rappa the "big name" anaye-own Bad Boys Ent Sean Puffy Combs aka Diddy amekubali matokeo na kumtumia salamu za pongezi rappa aliye-"make headlines" za mitandao kibao juzi kati baada ya kuripotiwa kuwa ndie anayeongoza kwa kuwa na mkwanja mrefu aka mapene aka pesa Sean Cutter aka Jay Z,wachambuzi wa masuala ya watu maarufu aka wadaku wamesema huo ni uungwana na ni kuonesha ni jinsi gani mchizi amekuwa mtu mzima sasa..hiyo ndio mambo...

SEAN CUTTER

Tuesday, August 31, 2010

NEW HIPHOP MAGAZINE..KITAANI SOON.

"AMEJIBU MAOMBI"-UPENDO NKONE..

THE BEAUTIFUL UPENDO NKONE

Baada ya kuishi mjane kwa miaka tisa sasa hatimaye maombi ya mwimbaji maarufu wa muziki wa injili Tanzania UPENDO NKONE ya kupata mume yamejibiwa...Upendo mmoja kati ya wahudumu wazuri nnaowa-admire sasa kufunga ndoa tar 17 mwezi ujao na mchumbake mpya Askofu wa Kanisa la Philadelphia Assembles Kigoma Baba John Mbeyela...."haya ni majibu niliyojibiwa na Baba Mungu Mwenyezi baada ya kuishi maisha magumu na ya upweke kwa muda wa miaka tisa baada ya mume wangu mpendwa kufariki dunia na ndugu wa mume wangu kuinyanyasa sana"..amesema Upendo ambaye hivi sasa yuko safi zaidi kimaisha kwa kufanikisha kupeleka watoto wake international schools, kujenga nyumba nzuri na kuwa na gari zuri la kutembelea baada ya mauzo manono ya albamu zake tatu ambazo ni "Mungu Baba", "Hapa Nilipo" na "Zipo Faida"...Huu ni ushuhuda kuwa AOMBAE HUPEWA..Hongera Upendo Nkone..MNM inakutakia mafanikio katika ndoa yako mpya.

UPENDO NKONE

MSALA WA MOZ DEF HUU HAPA..

MOS DEF

Huu ni msala ambao umekuwa ukiripotiwa sana kwenye vyombo vya habari wiki hii...kuwa rappa na mtayarishaji mahiri wa muziki wa Hiphop nchini Marekani Dante Smith aka Mos Def afikishwa kwenye mahakama ya Los Angeles County Superior Court kwa kuitapeli kampuni ya kuandaa matamasha REMG Ent kwa kushindwa kufika kwenye show yao ya Kool Haus huko Toronto Canada ambayo alikwishalipwa malipo ya utangulizi ya dolali za kimarekani 12,500...Moz Def ametakiwa kuilipa kampuni hiyo fidia ya dolali 57,500 baada ya kuisababishia hasara ya maandalizi ya zaidi ya dolali 45,000...so??hii tunajifunza nini???kuwa kumbe hata mbele washkaji wanaingiaga mitini baada ya kupokea kianzio cha show..sio BONGO tu..dah!!

ANATAFUTWA.....


MNM imeombwa msaada...no comment.....